Shirika la Habari la Hawza - Mkuu wa Jumuiya ya Walimu wa Seminari ya Qom Ayatollah Sayyid Hashem Hosseini Bushehri alitoa hotuba katika hafla ya kuhitimisha toleo la 26 la Kitabu cha Mwaka wa Seminari katika Seminari ya Imam Kadhim (a.s) huko katika Mji wa Qom, akisema: "Ayatollah Al-Udhma Shobeiri Zanjani anazingatiwa kuwa miongoni mwa waanzilishi wa enzi za sasa, na alithaminiwa (na kutunukiwa na kupewa heshima yake) katika kongamano hili."
Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Wataalamu amebainisha zaidi kuwa Hayati Ayatollah Rey Shahri pia alifanya juhudi za ikhlasi kwa miaka mingi katika nyanja mbalimbali hususan katika uga wa Hadithi ambapo pia alitunukiwa na kuthaminiwa katika kongamano hili.
Mkuu wa Jumuiya ya Walimu wa Seminari ya Qom aliendelea kwa kusema kuwa: “Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w) aliichukulia kalamu kuwa ni baraka kubwa iliyopelekea maendeleo ya Dini, Dunia na Maisha (ya Mwanadamu).
Your Comment